Mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize, yuko Afrika Kusini kwa ajili ya kupatiwa matibabu kufuatia kuumia tena akiwa mazoezini.
Mzize ambaye yuko nje ya uwanja kwa muda mrefu, aliumia tena muda mchache kabla timu yake haijasafiri kuelekea Lindi kuifuata Namungo mapema wiki hii.
Taarifa kutoka Yanga zimesema upo uwezekano mkubwa mshambuliaji huyo akafanyiwa upasuaji mwingine ili kutibu haraka jeraha linalomkabili.
“Tunavyozungumza tayari Mzize yuko Afrika Kusini, uamuzi wa kwenda huko umelenga kuharakisha matibabu yake, lakini pia kumweka katika nafasi nzuri ya kurejea uwanjani mapema,” kimesema chanzo chetu.
Chanzo; Nipashe