Mshambuliaji nyota wa Kenya, Michael Olunga, anaendelea kuthibitisha ubora wake ndani na nje ya uwanja baada ya kutajwa kuwa miongoni mwa wachezaji matajiri zaidi Afrika Mashariki, kufuatia mafanikio yake makubwa akiwa na klabu ya Al Arabi SC nchini Qatar.
Kwa mujibu wa taarifa za michezo, Olunga analipwa takribani euro milioni 5.8 kwa mwaka sawa na zaidi ya shilingi bilioni 17 za Kitanzania hali inayomweka kwenye orodha ya wachezaji wa Afrika Mashariki wanaolipwa mshahara mkubwa zaidi.
Mafanikio yake yanafananishwa na yale ya nahodha wa zamani wa Kenya, Victor Wanyama, huku Olunga akitajwa kuwa fahari ya soka la Kenya na mfano wa kuigwa kwa vijana wengi wa ukanda huu.
Chanzo; Global Publishers