Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bondia Antony Joshua Kustaafu Ngumi Baada Kunusurika Kifo

Bondia Anthony Joshua anatarajiwa kustaafu mchezo wa masumbwi baada ya kunusurika katika ajali mbaya ya gari iliyosababisha vifo vya marafiki zake.

Mjomba wa Anthony Joshua anayefahamika kwa jina la Ademola Johua amedai kuwa bingwa wa zamani wa dunia amewaeleza familia yake kuwa atastaafu ndondi kufuatia ajali mbaya ya gari iliyowaua marafiki zake wawili wa karibu.

Adedamola Joshua 
“Jambo kubwa zaidi ni kwamba atastaafu ndondi. Hilo ni jambo moja linalotufanya tufurahi kwa sababu kila anapopigana ulingoni, sisi huwa tunaguswa sana kihisia,” alisema mjomba wake,

“Kila anapoangushwa, ni kama moyo unatoka kifuani mwetu. Hisia zote hizo na maumivu kila anapopigana ni kiwewe kikubwa sana kwetu pia.

"Sasa kwa kuwa amesema atastaafu sisi kama ndugu zake hatuna budi zaidi ya kufurahi".

 

Chanzo; Bongo 5

 

 

 

Kuhusiana na mada hii: