Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Lamine Yamal Aondolewa Kikosi cha Hispania

Nyota wa Barcelona Lamine Yamal ameondolewa kwenye kikosi cha Uhispania kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Georgia na Uturuki chini ya kocha Luis de la Fuente.

Yamal alipaswa kuucheza mechi hizo mbili baada ya kuichezea Barcelona katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Celta Vigo Jumapili lakini sasa ameondolewa kwenye nafasi hiyo.

Meneja wa Barcelona Hansi Flick aliikosoa Uhispania kwa kumchezesha Lamine Yamal katika mechi ya kufuzu dhidi ya Bulgaria na Uturuki mwezi Septemba.

Alikosa mechi nne za Barcelona kutokana na jeraha la paja baada ya mapumziko hayo ya kimataifa na hakuwepo kwenye mechi za Uhispania dhidi ya Georgia na Bulgaria mnamo Oktoba.

Bado Barcelona wameweka wazi kwamba Yamal anatakiwa kupona kile kinachojulikana kuwa jeraha gumu, na sasa atapumzika vizuri wakati wa mapumziko ya kimataifa.

 

Chanzo; Bbc

Kuhusiana na mada hii: