Nyota wa Barcelona Lamine Yamal ameondolewa kwenye kikosi cha Uhispania kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Georgia na Uturuki chini ya kocha Luis de la Fuente.
Yamal alipaswa kuucheza mechi hizo mbili baada ya kuichezea Barcelona katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Celta Vigo Jumapili lakini sasa ameondolewa kwenye nafasi hiyo.
Meneja wa Barcelona Hansi Flick aliikosoa Uhispania kwa kumchezesha Lamine Yamal katika mechi ya kufuzu dhidi ya Bulgaria na Uturuki mwezi Septemba.
Alikosa mechi nne za Barcelona kutokana na jeraha la paja baada ya mapumziko hayo ya kimataifa na hakuwepo kwenye mechi za Uhispania dhidi ya Georgia na Bulgaria mnamo Oktoba.
Bado Barcelona wameweka wazi kwamba Yamal anatakiwa kupona kile kinachojulikana kuwa jeraha gumu, na sasa atapumzika vizuri wakati wa mapumziko ya kimataifa.
Chanzo; Bbc