Kwa mara nyingine Simba imeshindwa kupata ushindi katika mechi ya hatua ya makundi baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya wenyeji, Atletico Petroleois ya Angola.
Katika mechi hiyo iliyochezwa mjini Luanda, Simba ilienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0.
Pedro Pinto aliwatanguliza wenyeji kwa kufunga bao dakika ya 13, goli lililoanza kuzamisha ndoto za Simba kupata ushindi katika mchezo huo wa raundi ya tano.
Kiungo mshambuliaji mpya wa Wekundu watakuwa Msimbazi, Anicet Oura, aliisawazishia timu yake dakika ya 81.
Matokeo hayo yanaifanya Simba kuvuna alama ya pili katika hatua ya makundi ikibakisha mchezo mmoja wa kukamilisha ratiba nyumbani dhidi ya Stade de Malien ya Mali.
Chanzo; Nipashe