Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Messi Awekwa Kando Pre Season

Klabu ya Inter Miami imethibitisha kuwa nyota wao, Lionel Messi, atakosa mazoezi ya siku kadhaa za maandalizi ya msimu mpya ‘Pre Season’ kufautia majeraha ya misuli (muscle strain) ya nyuma ya paja la mguu wa kushoto yanayomsumbua kwa sasa.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu hiyo, Messi alifanyiwa vipimo vya ziada vilivyothibitisha tatizo hilo.

Kurejea mazoezini kwa mshambuliaji huyo raia wa Argentina kutategemea maendeleo yake kiafya na tathmini ya kitabibu katika siku zijazo.

Habari hiyo imeibua wasiwasi kwa mashabiki wa soka duniani, huku wengi wakimtumia salamu za kumtakia nafuu ya haraka nahodha huyo wa Argentina.

Tunamtakia Messi apone haraka na kurejea uwanjani akiwa imara zaidi.

 

 

 

Chanzo; Mwanaspoti

Kuhusiana na mada hii: