Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mo Salah Ampiku Gerrard kwa Asisti Liverpool

Mohamed Salah amempiku gwiji na nahodha wa zamani wa Liverpool, Steven Gerrard kwa kufikisha asisti 93 kwenye Ligi Kuu England ndani ya klabu hiyo.

Mo Salah alifikisha idadi hiyo ya asisti wakati alipomtengenezea bao pekee na la ushindi, Virgil van Dijk kwenye ushindi wa Jumatano usiku wa Liverpool wa 1-0 dhidi ya Sunderland.

Ryan Giggs anaongoza katika orodha ya wachezaji wenye asisti nyingi zaidi kwenye Ligi Kuu England akiwa na 162, huku Kevin De Bruyne (119) akishika nafasi ya pili na Cesc Fabregas (111) akiwa nafasi ya tatu.

Wengine kwenye 10 bora ni Wayne Rooney (103), Frank Lampard (102), Dennis Bergkamp (94), David Silva (93), Mohamed Salah (93), Steven Gerrard (92) na James Milner (90).

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: