WAKATI Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), likisogeza mbele kuanza kwa mechi za msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL), wababe wa ligi hiyo Simba na Yanga zenyewe zitauaga mwaka 2025 kwa kuvaana katika Dabi ya Kariakoo Desemba 28.
Awali ligi hiyo iliyozinduliwa mwezi uliopita kwa mechi za Ngao ya Jamii, ilipangwa kuanza jana Alhamisi, lakini sasa imetangazwa imesogezwa mbele hadi Novemba 14 kwa kupigwa michezo minne, huku mbili za raundi ya kwanza zikipangwa Desemba 8.
Mechi ya watetezi wa taji la Ligi hiyo, JKT Queens waliokuwa wanaanze Novemba 8 dhidi ya Bunda Queens mechi hiyo imewekwa kiporo hadi Desemba 8 kutokana na muingiliano wa ratiba ya Ligi ya Mabingwa Afrika inayonza Misri wakiwa ni washiriki.
Chanzo; Mwanaspoti