Wafuasi wa CHADEMA wamejitokeza katika Mahakama Kuu ya Tanzania Masijala Ndogo ya Dar es Salaam kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa chama hicho Tundu Lissu.
Wafuasi hao pia wamefanya maombi ndani ya chumba cha mahakama kabla ya kuanza kwa kesi hiyo ambayo inatarajiwa kutolewa uamuzi mbele ya Jopo la Majaji watatu akiwemo Jaji Dunstan Ndunguru.
Uamuzi huo unatokana na mapingamizi ya Lissu ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho ya kumpinga shahidi wa Nne ambaye ni wa siri kutoka upande wa Jamhuri.
Chanzo; Millard Ayo