Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Ccm Yalaani Vitendo vya Uvunjifu wa Amani

Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya chama tawala nchini Tanzania CCM imelaani vitendo ilivyovitaja kuwa vya kihuni na uvunjifu wa amani vilivyofanywa na baadhi ya watu vilivyosababisha vifo na uharibifu wa mali za umma na za wananchi.

Hata hivyo taarifa ya kamati hiyo haikugusia madai ya mauaji yaliyofanyika wakati wa maandamano ya uchaguzi na kutajwa na mashirika tofauti yakiwemo ya utetezi wa haki za binadamu na chama cha upinzani Tanzania CHADEMA.

Aidha pia kamati hiyo iliyokutana leo mjini Dodoma katika kikao maalum cha kutafakari hali ya kisiasa baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, imewapongeza wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi.

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: