Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Nape Awavaa Wanaohoji Utu wa Samia

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama Mkoani Lindi Nape Moses Nnauye amesema kuwa wanaohoji imani na dhamira ya Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kusimamia utu wa Watanzania ni Watu walioamua kujitoa akili, wakidhamiria kuwavuruga na kuwadanganya Watanzania wapenda utu na maendeleo ya Nchi yao Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu.

Nnauye amebainisha hayo leo Jumatano Septemba 24, 2025 kwenye Viwanja vya Mtama wakati wa mkutano wa kampeni za Dkt. Samia, akibainisha kuwa tangu kuingia madarakani kwa Rais Samia, matendo, maelekeo na maneno yake mengi yamekuwa yakionesha dhamira yake njema katika kukuza, kustawisha na kuheshimisha utu wa Mtanzania kupitia huduma muhimu za kijamii pamoja na ustawi wa kiuchumi na kijamii.

 

Chanzo Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: