Mahakama Kuu nchini Afrika Kusini imetupilia mbali rufaa iliyowasilishwa Jumanne na familia ya aliyekuwa Rais wa Zambia, Edgar Lungu, iliyokuwa ikitaka kusitisha urejeshaji wa mwili wake nchini Zambia kwa mazishi.
Familia hiyo ilifikisha suala hilo katika Mahakama ya Pretoria kupinga uamuzi wa awali ulioruhusu serikali ya Zambia kurejesha mwili wa Lungu nchini humo kwa mazishi ya kitaifa.
Familia ilikuwa na matumaini ya kupeleka suala hilo katika Mahakama ya Rufaa ya Juu (SCA), lakini ombi lao lilikataliwa na mahakama hiyo, sambamba na amri ya kulipa gharama za kesi.
Mahakama ilisema kuwa hakukuwa na uwezekano wa mafanikio kwa rufaa hiyo.
Chanzo; Global Publishers