Wakati Chama Cha Mapinduzi, CCM, chama tawala nchini Tanzania, kinaadhimisha miaka 49 tangu kuasisiwa kwake, maadhimisho hayo yanafanyika katika mazingira ya maswali mazito na mjadala mkali wa kisiasa.
Ni chama kinachojivunia miongo ya uongozi, lakini pia kinachokabiliwa na ukosoaji mkubwa kufuatia ghasia za uchaguzi zilizoigharimu nchi maisha ya raia kadhaa.
Je, CCM iko tayari kwa maridhiano ya kitaifa? Mwandishi wetu Yakub Talib amezungumza na Msemaji Mkuu wa CCM, Kenan Kihongosi. Lakini kabla ya hilo, anaangazia mafanikio ambayo chama hicho kinasema kimeyapata katika miaka 49 ya uongozi wake.
Chanzo; Dw