wenyekiti Ngome ya Vijana ACT Wazalendo - Abdul Nondo leo amehoji juu ya Tsh. Bilioni 200 ambazo ni fedha alizitoa Mh.Rais Samia mwaka huu Januari
2026 kwa ajili ya kuwezesha vijana kupata mikopo.
Hata hivyo Waziri wa Maendeleo ya Vijana Mh. Joel Nnanauka amesema kuwa fedha hizo tayari zimetolewa na zimepelekwa wizara za kisekta kama Wizara ya Kilimo; Wizara ya Mifugo na Uvuvi; Wizara ya Madini; Wizara ya Viwanda na Biashara; Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.
Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo, wametaka kupata ufafanuzi juu ya utaratibu unaotumika na wizara hizo za kisekta katika utolewaji na ukopeshaji wa hizi fedha bil. 200 kwa vijana pamoja na muongozo unaotumika katika ukopeshaji wa hizi fedha katika hizo wizara za kisekta ili vijana wote wenye sifa na vigezo wapate na wajue taratibu za kukopa na kurejesha fedha hizo.
Chanzo; Clouds Media