Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Gari la Mgombea Urais Lapigwa Jiwe Mafinga

Gari analotumia Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha CHAUMMA Salum Mwalim, limepigwa jiwe kwenye kioo cha nyuma na Mtu asiyejulikana muda mfupi baada ya kumshusha Mgombea huyo Hotelini Mafinga, Mkoani Iringa.

Mkuu wa msafara huo, John Mrema amesema tukio hilo limetokea usiku huu wakati Wasaidizi wa Mgombea walipotoka kutafuta chakula na huduma za dawa, ndipo mawe yaliporusha dhidi ya gari hilo na kuharibu kioo hicho ambapo OCD wa Mafinga amesema Polisi wamewakamata Watu wanne kuwahoji kutokana na tukio hilo.

Gari hili ni miongoni mwa Magari yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi kusaidia usafiri wa Wagombea urais katika kipindi cha kampeni.

 

Chanzo: Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: