Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Starlink Yasitisha Hudama za Intaneti Uganda

Mtoa huduma wa intaneti ya setilaiti, Starlink, amesitisha upatikanaji wa mtandao wake wa kimataifa nchini Uganda.

Hatua hiyo imesababisha vifaa vyote vya Starlink vilivyokuwa vinatumika nchini humo kusitisha kazi kuanzia Januari 1, 2026, kufuatia agizo la Tume ya Mawasiliano ya Uganda (UCC) kuhusu matumizi ya huduma za setilaiti zisizo na leseni.

Katika barua ya Januari 2, mwaka huu, Starlink ilithibitisha iliwasilisha na kuanzisha mfumo wa kuzuia huduma ili kuzuia kabisa upatikanaji wa intaneti ya setilaiti ndani ya Uganda.

Barua hiyo, iliyosainiwa na Ben MacWilliams, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Teknolojia ya Utafiti wa Anga, ilielekezwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa UCC, ikiwa ni majibu ya hoja zilizotolewa kuhusu matumizi haramu ya huduma za intaneti ya setilaiti nchini humo.

Starlink inaeleza kuwa haiuzi, haitangazi wala haitoi moja kwa moja huduma za intaneti ya setilaiti nchini Uganda, na kwamba hakuna vifaa vya Starlink vilivyoingizwa au kusambazwa rasmi nchini humo.

“Ili kuweka wazi, Starlink Uganda yenyewe haiuzi wala haitangazi huduma za intaneti ya setilaiti nchini Uganda kwa kuwa bado haijapatiwa leseni na UCC,” inaeleza kampuni hiyo.

Kwa mujibu wa Starlink, upatikanaji wa huduma hiyo nchini Uganda kabla ya kusitishwa uliwezeshwa kupitia vifaa vilivyonunuliwa na kuanzishwa matumizi katika nchi ambazo Starlink imeidhinishwa kisheria, kisha baadaye kuingizwa Uganda bila ruhusa.

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: