Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema Februari 8, 2026 Rais Samia Suluhu Hassan atazindua Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Chalamila amewataka wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa soko hilo.
Pamoja na hayo amewataka wafanyabiashara wote walioziba barabara za kuingia sokoni hapo kuziachia.
Mkuu huyo wa mkoa ametoa tamko hilo leo Ijumaa, Februari 6, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Chanzo; Mwananchi