Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

TRA Yazindua Mfumo Mpya wa Ulipaji Kodi

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) amezindua mafunzo ya mfumo mpya wa kidijitali wa Integrated Domestic Revenue Administration System (IDRAS) kwa wadau wa kodi, yanayofanyika kwa muda wa siku tatu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kuzindua mafunzo hayo, Kamishna Mwenda amesema mfumo huo utaondoa malalamiko mengi kutoka kwa wadau na walipakodi, kwa kuwa utawezesha huduma kupatikana saa 24 kwa siku, huku mtumiaji akiwa na uwezo wa kuutumia popote alipo kupitia simu au kifaa kingine cha kielektroniki.

Ameongeza kuwa mfumo wa IDRAS pia utawawezesha wafanyabiashara kutoa risiti za kielektroniki za EFD hata pale ambapo hawana mashine za EFD katika maeneo yao ya biashara.

Kwa mujibu wa Kamishna Mwenda, hatua hiyo inalenga kurahisisha ulipaji wa kodi, kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato na kuboresha mazingira ya biashara nchini.

 

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: